TANGAZO KWA UMMA - UFADHILI WA MASOMO YA UZAMILI KADA YA AFYA.

Labels:

MoHCDGEC

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO   
   
                                                         TANGAZO KWA UMMA 
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto anawatangazia watumishi wote waliopata udahili wa kusoma masomo ya Shahada ya Uzamili (Masters Degree) katika fani za Afya kwa mwaka 2019/2020, kwamba Wizara inapokea maombi ya Ufadhili kwa mwaka 2019/2020. Maombi haya yatawasilishwa kwa njia ya kielektroniki kwa kutumia link iliyotolewa kwenye tangazo hili. Maombi yatakayofanyiwa kazi ni yale yatakayowasilishwa kwa njia ya mfumo huu tu, hivyo waombaji waliowasilisha maombi yao kabla ya tangazo hili wanapaswa kufuata utaratibu huu.
Ufadhili huu ni kwa ajili ya kulipiwa ada ya mafunzo (Tuition fee), pamoja na posho ya utafiti pindi mwanafunzi anapokuwa kwenye kipindi cha kufanya utafiti kama sehemu ya mafunzo yake (Dissertation Allowance). Malipo ya posho ya utafiti yatazingatia viwango vilivyopitishwa na Wizara.
Vigezo vitakavyotumika kuchagua watakaowasilisha maombi yao ni hivi vifuatavyo :
1. Kuwasilishwa kwa maombi rasmi ya ufadhili kwa njia ya mfumo (Post-graduate Sponsorship Online Application System)
2. Mwombaji awe Raia wa Tanzania.
3. Awe amedahiliwa Chuoni kuanza masomo kwa mwaka wa kwanza 2019/2020
4. Mwombaji awe amefanya kazi kwa muda usiopungua miaka miwili baada ya kuajiriwa serikalini.
5. Kipaumbele kitatolewa kwa: a. Watumishi wa Serikali waliomo kwenye sekta ya Afya wanaofanya kazi katika vituo vilivyoko Wilayani/Mikoanii pamoja na  Hospitali za Rufaa za Mikoa ambao baada ya mafunzo watarudi kuendelea kufanya kazi katika vituo vyao vya awali, au watapangiwa vituo vya kazi sehemu nyingine yeyote nchini yenye uhitaji. b. Waombaji waliodahiliwa katika fani ambazo ni za msingi katika utoaji wa huduma za rufaa katika Hospitali za Rufaa za Mikoa. Nyanja hizo ni Anaesthesiology, Surgery, Obstetrics and Gynaecology, Orthopaedics
 Surgery, Emergency Medicine, Paediatrics, Internal Medicine, Neurosurgery,Radiology, Oncology,Opthalmology, ENT,Psychiatry, Microbiology,  Critical Care in Nursing na Midwifery and Womens Health, Clinical Pharmacy, Pharmaceutical Management, Epidemiology and Lab.Management. c. Waombaji waliodahiliwa katika nyanja za Ubingwa wa Juu (Super-specialities) zenye umuhimu mkubwa katika Hospitali Maalumu, Kanda na Kitaifa (kama Cardiology, Nephrology,Haematology,Endocrinology, Neurology, Pulmology, Gastroentorology, Radiography) ili kujenga uwezo wa ndani ya nchi katika jitihada za kupunguza wagonjwa wa rufaa wanaotibiwa nje ya nchi.
6. Aidha, mwombaji atatakiwa awe ameambatisha nyaraka zifuatazo wakati wa kufanya maombi: a. Barua ya ruhusa ya masomo kutoka kwa mwajiri wake b. Barua ya udahili kutoka chuoni c. Cheti cha taaluma d. Cheti cha kuzaliwa

Maombi yote yawasilishwe kwa kutumia ‘link’ ifuatayo:             
esponsorship.moh.go.tz
Mwisho wa kupokea maombi haya ni tarehe  16/11/2019.
 
Imetolewa na:
Katibu Mkuu, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mji wa Serikali Mtumba,                                     
 Barabara ya Afya,   S. L. P. 743               
40478 DODOMA 18/10/2019   
   

0 comments: